Featured
Loading...

JE BADO UJAPATA WAZO LA BIASHARA: BOFYA HAPA UPATE MAWAZO (150) YA BAISHARA


Watu wengi wamekuwa wakiangaika hama kuwauliza watu wao wa karibu ni biashara gani afanye au ukimuuliza ni biashara gani unataka kufanya atakuambia mimi nataka kufanya biashara yoyote ili mradi tu iwe inaniingizia faidi. Kuwa maalum(specific) na usipende kufanya biashara yoyote kwani kama ujui unataka kwenda wapi basi uelekeo wowote utakupeleka usipotaka. Si mawazo yote yatakuwa sawa kwako,chagua wazo moja tu la biashara  na uanze kulifanyia kazi na uanze sasa kwa kutumia chochote ulichonachoo usingoje kuwa na fedha nyingi ndiyo uanze.Chagua eneo gani upo vizuri na kuchukua hatua sasa.


 1.Kununua Mashine za kukoroga zege na kukodisha.

2.Kununua Mashine za kukata vyuma na kuzikodisha.

3.Kutengeneza na kuuza tofali.

4.Ufundi, Website updating/Database: Katika Halmashauri, Manispaa, Mashule, Wizara, Wilaya na Makampuni mbalimbali.

5.Kuanzisha kituo cha redio na televisheni.

6.Kufunga na kutengeneza vifaa mbalimbali vya electroniki na mawasiliano mfano; compyuta na vifaa vya compyuta na mawasiliano.

7.Kuuza software; mfano Antivirus, Operating Systems, Pastel, Tally, Myob, n.k

8.Kushona na kuuza nguo.

9.Kufungua Duka la kuuza nguo mpya; suit, socks, batiki, nguo za asili, Mashuka, Mashati, Suruali.

10.Ufugaji wa mifugo mbalimbali mfano Kondoo, Mbuzi, Ng?ombe, Kuku, Bata, na wengine.

11.Kufungua stationery, kuuza (supply) vitabu na vifaa mbalimbali ktk mashule na vyuo.

12. Kutoa ushauri mbalimbali waKitaalamu.

13.Kuuza viazi, mahindi, mihogo, kutengeneza popcorn na kuziuza.

14.Kusajili namba za simu na kuuza vocha

15.Kuwa na mradi wa Pikipiki zisizotumia mafuta na zinazotumia mafuta

16. Kilimo cha mazao mbalimbali kulingana na hali ya hewa ya sehemu husika.

17.Kuuza Mitumba.

18.Kusimamia miradi mbalimbali

19.Kufungua duka la kuuza mitambo mbalimbali.

20.Kufungua banda la chakula na chips.

21.Kukodisha turubai viti na meza.

22.Kufungua Supermarket.

23.Kufungua Saluni.

24.Kufungua Bucha.

25.Video Shooting & Editing.

26. Kufungua Internet cafe.

27.Duka la kuuza matunda.

28.Kufungua duka la kuuza vifaa vya simu za mkononi na landline.

29.Kufungua duka la vifaa vya ujenzi; cement, vifaa vya umeme, duka la mabati.

30.Kutengeneza michoro mbalimbali ya majumba na miradi ya ICT.

31.Kuchapa vitabu, bronchures, n.k32.Kuanzisha kampuni ya ujenzi (Building contractor).

33.Kuuza Vifaa vya umeme wa nishati ya jua (solar) ,battery, inverter na vifaa vingine vya solar n.k.

34.Kuuza maji kwa jumla na rejaleja.

35.Kutengeneza na kuuza Unga wa lishe bora.

36.Kukodisha Music

37.Kuanzisha Mradi wa Taxi

38. Kuanzisha mradi wa Daladala.

39.Kuuza vifaa vya Kompyuta, laptops, converters, HDDs, Monitors, Softwares, CD Copiers na vifaa vingine.

40. Kununua magenerator na kukodisha

41.Kufungua kampuni ya kutoa huduma za simu.

42. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za internet (ISP).

43.Kuuza mabati na vigae

44.Kujenga apartments

45. Kufungua Kisima cha mafuta ya taa au mafuta ya aina zote.

46.Kufungua Duka la samaki.

47.Kufungua Duka la nafaka.

48.Kufungua Shule za Awali, Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo.

49.Kujenga hostel

50.Kuuza vocha na vingamuzi vya DStv, Zuku, Startimes, Easy TV, TNG, Digitech, Continental.

51.Kujenga mtambo wa kuzalisha umeme na kuuza katika viwanda na wananchi.

52.Ufundi simu

53.Kufungua Hospitali, Zahanati.

54.Maabara ya Macho, Meno

55. Kuchimba/Kuuza Madini

56.Kufungua ofisi ya kutoa huduma ya simu na fax.

57.Kuuza miti na mbao.

58.Kufungua Grocery, bar

59.Kufungua studio ya kupiga na kusafisha picha.

60.Kucharge simu/battery.

61.Duka la TV na vifaa vingine.

62.Kuanzisha biashara ya kuuza vyakula katika sherehe na tamasha mbalimbali (catering).

63.Banda la kupigisha simu.

64.Kuuza na kushona Uniform za shule.

65.Kuanzisha duka la kuuza vitu kwa jumla.

66.Kufungua gereji za kutengeneza bajaji, pikipiki na magari

67.Kuuza vyuma, pembejeo, rake, jembe

68.Kuuza fanicha.

69.Kufungua sehemu ya kuziba pancha za matairi ya magari na mitambo.

70.Kujenga nyumba za kulala wageni (hotel)

71.Kuagiza na kuuza vifaa vya aluminium.

72.Kuuza vioo

73.Kushona na kukodisha nguo za harusi.

74.Kufungua yard kwa ajili ya kuosha magari

75.Kuuza mashine za kuchomelea (welding machine).

76.Kuuza vifaa vya kuvaa Site (boots, helmets etc)

77.Kununua mabasi kwa ajili ya kusafirisha wanafunzi

78.Kufungua studio ya kutengenezavipindi vya redio na televisheni

79.Kuanzisha ofisi ya michezo ya televisheni (TV Games)

80.Kufungua benki.

81.Kuwa na malori ya kubeba kokoto na mchanga.

82.Kuuza vifaa mfano TV, CCTV Camera, n.k

83.Kuwa dalali wa vitu mbalimbali.

84.Kuanzisha mradi wa kukodisha fork lift na winchi (crane)

85.Kuanzisha kiwanda cha kutengeneza viatu.

86.Kuanzisha viwanda mbalimbali

87.Duka la vifaa vya simu na gadgets mbalimbali zinazoendana na mawasiliano ya Vodacom, TTCL, AIRTEL, TIGO, ZANTEL, n.k.

88.Kujenga Ukumbi wa kukodisha kwa sherehe, mikutano mbalimbali

89.Kununua matrekta, mitambo ya ujenzi wa barabara na kukodisha

90.Kutengeneza antenna na kuuza

91.Kufungua mradi wa Machine za kusafisha, kutoboa na kuchana mbao

92.Kufungua mradi wa kuuza vifaa vya Umeme wa kutumia upepo

93.Biashara ya kuagiza magari

94.Kufanya biashara za Jukebox

95.Kukodisha matenki ya maji

96.Kufungua duka la kuuza Asali

97.Kutengeneza Mikokoteni/ matoroli na kuikodisha

98.Kufungua Duka la vinyago, batiki

99.Kuanzisha huduma ya AIRTEL MONEY, MPESA, TIGOPESA, EZYPESA

100.Kuanzisha sehemu ya kufanyia mazoezi (Gym).

101.Kununua na kuuza vifaa vya kupima ardhi.

102.Kufungua duka la kuuza dawa (pharmacy).

103.Kufungua Kampuni ya Ulinzi

104.Kufungua kampuni ya"Clearing and fowarding"

105.Kuchezesha vikaragosi

106.Kuuza spea za bajaji, magari na pikipiki

107.Kuuza baiskeli

108.Kuuza magodoro

109.Kuuza vyombo mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya nyumbani mfano bakuli, sahani, vikombe,vijiko,

110.Kuuza marumaru (limestones)

111.Kuuza kokoto

112.Kuuza mchanga

113.Kufundisha Tuisheni

114.Biashara za bima

115.Kampuni ya kusafirisha abiria kwa njia ya anga (ndege)

116.Biashara za kitalii

117.Biashara za meli na maboti.

118.Kampuni ya kuchimba visima

119.Kufungua ofisi ya wakili/mawakili wa kujitegemea

120.Kuuza mkaa

121.Kutengeneza mashine za kutengeneza tofali

122.Kampuni ya kupima ardhi

123.Kampuni ya magazeti

124.Kuchapa (printing) magazeti

125.Kuuza magazeti

126.Kuchimba mafuta

127.Kiwanda cha kutengeneza mabati

128.Kiwanda cha kutengeneza fanicha

129.Kiwanda cha kutengeneza matairi

130.Kutengeneza vitanda vya chuma

131.Kununua nyumba katika Maghorofa (Apartments) na kuzikodisha.

132.Kukodisha makapeti

133.Kupamba maharusi na kumbi za harusi/sherehe.

134.Mashine ya kusaga na kukoboa nafaka.

135.Kazi ya ususi na kusafisha kucha.

136.Kuuza Gypsum

137.Malori ya kubeba mafuta na Mizigo

138.Duka la kuuza mboga za majani

39.Duka la kuuza maua.

140.Kampuni ya kuzoa takataka

141.Kampuni ya kuuza magari

142.Kuuza viwanja

143.Uvuvi

144.Kutengeneza na kuuza nguzo za kujengea fensi

145.Uchoraji wa mabango.

146.Duka la kuuza silaha

147.Ukumbi wa kuonesha mpira

148.Biashara ya Multi-Level Marketing-MLM

149.Yadi kwa ajili ya kupaki magari

150.Mradi wa trekta za kukodisha kwa ajili ya kilimo..

Amua haraka nini unataka kufanya nini kwa ajili yako na maisha yako na kama kweli unataka kufanya biashara/ujasiriamali  napenda kukusisitiza uanze sasa kwa kutumia chochote ulichonacho kwani ndege mmoja aliyo mkonono mwako ni bora zaidi kuliko 100 walio angani.

Namna Ya Kuona Fursa Na Kuzinyakua.

.
Katika maisha yetu ya kila siku neno fursa si geni sana masikioni mwetu.Neno hili watu wengi hulichukulia kama la kawaida sana lakini kiukweli kama utaweza kujua maana yake na kufanyia kazi lazima utaona mabadiliko makubwa katika maisha yako.Fursa nyingi hapa duniani zinakuwa haziko wazi au kwa maneno mengine zinakuwa zimejificha sana.Leo hii nataka nikushirikishe njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuona fursa mbalimbali katika eneo lako.


1.Tambua fursa ikoje
Ili uweze kuona fursa katika maisha lazima ujue kwanza fursa ni nini na inafananaje.Kwa mfano unaweza ukawa unatafuta kitu fulani lakini kwenye akili yako lazima ujenge picha ya kile kitu unachokitaka.Kwa kufanya hivi inakuwa rahisi kwa mtu kujua ni nini hasa anakitaka na atumie mbinu gani na muda gani ili aweze kufanikisha.

2.Otesha mbegu nyingi
Kuna msemo usemao usiweke mayai yote kwenye kapu moja.Kama unataka kuwa na fursa nyingi ,anza kufanya vitu vidogovidogo vingi na angalia ni kipi kinakuwa kikubwa.Kama kila kitu kitakuwa na mpango mmoja na hamna mipango mingine B,C,D au E basi utakuwa hatarini sana na pengine mpango A unaweza usifanikiwe.


3.Uwe na vigezo vinavyoeleweka
Kwa vile fursa ziko kila mahali kama unazitafuta unapaswa kuwa na vigezo zipi nichukue na zipi niache.Jiulize maswali kama;
i)Itanifikisha karibu au mbali na malengo yangu?
 ii)Itanipa faida?
iii)Gharama gani zitahusika?
iv)Itafungua milango kwa mambo makubwa au itanipoteza?
v)Kama itafungua milango je nilikuwa nimejopanga kwa hilo?
vi)Je nikikataa hii fursa nitafunga fursa nyingine mbeleni?

4.Usidharau fursa ndogondogo
Watu wengi waliofanikiwa hapa duniani walianza kufanyia kazi fursa ndogondogo zilizohitokeza machoni mwao.Kwa kuanza na fursa ndogo inakifanya upate akili ya kupambana na kuona fursa kubwa.Unaweza ukawa na fursa ndogondogo tatu kwa wakati mmoja lakini mojawapo ndo ikakufaidisha na zile nyingine zikawa zimekuongezea maarifa ya kupambana.

5.Kuwa tayari
Ili uweze kuona fursa na kuinyakua lazima uwe na utayari wa kuipokea pindi inapojitokeza.Ebu fikiria kwa kina fursa kubwa imejitokeza;je utatumia muda wa kazini?utaweza kujikimu kiuchumi?majukumu gani mtu mwingine anaweza kuyafanya kwa muda mfupi-akuangalizie watoto,aangalie nyumba yako?.Kama hivi vinakufanya uchanganyikiwe,utawezaje kunyakua fursa ikijitokeza?

Nakutakia kila la kheri kwenye safari yako ya mafanikio ambayo umeianza rasmi. Hakuna kinachoshindikana kama kweli utaamua leo. 

UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI KAMA MRADI



MAHITAJI

Kuku(tetea) 10 na Jogoo 01
Banda bora
Vyombo vya chakula na maji
Chakula bora
Madawa na chanjo kwajili ya magonjwa
Chanzo cha nishati joto na mwanga
Elimu na ujuzi wa malezi bora
Chombo au chumba cha kutunzia vifaranga
Mayai ya kuku wa kisasa/mayai mabovu(ambayo hayakuanguliwa)
Madaftari au kitabu cha kutunzia kumbukumbu
KUKU 10

Wakati wa kuanza mradi wako hakikisha una kuku 10 (matetea) wenye umri sawa na hawajawai kutaga hata mara moja. Chagua kuku wenye rangi nzuri kutoka katika familia bora kutegemea malengo ya mradi wako. Mfano kama lengo lako ni kuzalisha kuku wa kienyeji kwajili ya nyama basi chagua mbegu ambayo inakuwa haraka na yenye uzito mkubwa. Au ikiwa lengo ni mayai basi ni vema kuchagua aina ya kuku yenye kukua haraka na kutaga mayai mengi.

Ili kupunguza gharama za manunuzi ya kuku na hivyo kuongeza faida kwa mfugaji ni vema kununua kuku wadogo ambao wametoka tu kuachishwa kulelewa na mama zao. Kuku hawa utawapata kwa bei ya chini, tena watafaa sana maana watakua na umri mmoja pia.

JOGOO 01

Jogoo mmoja tu anatosha kuwahudumia kuku matetea yote kumi. Hakikisha katika uchaguzi wa jogoo bora lililochangamka, rangi mzuri, upanga umesimama, macho angavu, uzito wa kutosha, rangi nzuri na uwezo mkubwa wa kuzalisha. Ni vema mfugaji akaelewa kwamba kuku wote watakaozalishwa watategemea ubora wa jogoo wake. Uwezo wa kutaga kwa kuku na upatikanaji wa mayai pia hutegemea kwa karibu ubora wa jogoo aliyechaguliwa.

BANDA BORA

Miongoni mwa mambo mhimu naya kwanza kuzingatiwa katika ufugaji wa kuku wa kienyeji kama mradi ni maandalizi ya banda bora. Kuku huhitaji banda bora ili wasiathirike na madhara mbalimbali. Mfugaji anatakiwa kuandaa banda lenye ukubwa wa mita 10 kwa mita 04. Yani urefu uwe mita 10 na upana upana wa mita 04. Kisha kata vyumba vya mita 2 urefu na upana mita 4 kutoka katika banda lako hivyo utakuwa na jumla ya vyumba vitano vyenye ukubwa unaolingana. Ujenzi uzingatie malighafi na vifaa vinavyopatikana kwa urahisi katika mazingira husika. Mfano katika maeneo ambayo fitoKuku zinapatikana kwa urahisi banda linaweza kuandaliwa kwa miti na kukandikwa kwa udongo. Au sehemu ambayo mabanzi hupatikana kwa urahisi basi banda laweza kujengwa kwa kutumia mabanzi. Vifaa vya kujengea banda vizingatie pia gharama na upatikanaji wake katika eneo husika. Baadhi ya vifaa hivyo ni kama ifuatavyo:-

Sakafu: Saruji, udongo, mbao, mianzi au fito
Kuta: Fito, mabanzi, mbao, nguzo mianzi,udongo, matofali, mawe, mabati na wavu
Paa: Nyasi, makuti, majani ya migomba, mabati na vigae.
Wigo: Matofali, mbao, fito nguzo, mabanzi, mianzi, matete, wavu na mabati
Banda bora la kuku linatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:-

Imara, lenye uwezo wa kuwahifadhi kiafya na pia dhidi ya hali ya hewa hatarishi kwa mfano jua kali, upepo, baridi na mvua pamoja na wanyama hatari.
Lenye mwanga, hewa na nafasi ya kutosha inayoruhusu usafi kufanyika kwa urahisi.
Lijengwe sehemu yenye mwinuko isiyotuama maji, isiyo na upepo mkali na iwe mbali kidogo na nyumba ya kuishi watu.
Liwe na vichanja kwa ajili ya kuku kupumzika na kulala.
Liwe na sehemu ya kuwekea chakula, maji, kutagia, kuatamia na sehemu ya kulelea vifaranga.
Liwe na nafasi ya kutosha kulingana na idadi ya kuku na kuweka vyombo vya chakula na maji.
Kwenye mazingira ya joto banda liwe la ukuta mfupi na sehemu kubwa wazi yenye wavu hadi kufikia kwenye paa. Kwenye mazingira ya baridi banda liwe na ukuta mrefu unaokaribia paa na sehemu ndogo tu iwe wazi yenye wavu ili kupitisha hewa na mwanga.
JINSI YA KUFANYA

Wakuze kuku wako hadi watakapofikia muda wa kutaga. Wakianza kutetea ni kiashiria kwamba wakati wa kutaga umekaribia hivyo andaa viota kwajili ya kutagia.

Viota vinapaswa viwe na ukubwa stahiki ili kumwezesha kuku kuyafunika mayai yote vizuri wakati wa kuetamia, viota viwe vinavyozuia mayai kutawanyika, viwe mahali pakavu na safi.

Hakikisha kuku wote wanataga katika viota tofauti. Kuku anapotaga IMG_20140306_153739mayai matatu unapashwa kuchukua mayai mawili na kumwachia yai moja ili kumfanya aendelee kutaga zaidi. Kuku akifikia yai la kumi na mbili anza kumwachia mayai matatu ili kumwandaa kwa kazi ya kuetamia. Kwa kufanya hivi, kuku atataga mayai 15 au zaidi na ikiwa atataga mayai 15 au chini ya hapo nakushauri utafute mayai mengine ujazilizie ili kufikisha mayai 20 kwa kila kuku. Zingatia kwamba mayai unayoyatoa kwa kila kuku, yanatunzwa sehemu salama, mahali pakavu, pasafi na penye joto la wastani.

Kuku wote wanapaswa kuanza kuetamia kwa siku moja. Ili kufanikisha hili inapasa uwe karibu na kuku wako. Kuku mmoja akianza kuetamia mwekee mayai ya kuku wa kisasa au mayai mabovu ya kuku wa kienyeji. Utafanya hivi hadi kuku wako wote watakapoanza kuetamia mayai. Kuweka mayai mabovu au mayai ya kuku yaliyotumika humfanya kuku aendelee kuetamia akijua ni mayai yake.

Baada ya kuona kwamba kuku wako wote wapo tayari kwa kuetamia mayai, waandalie banda maalumu kwajili ya kuetamia yani chumba kimoja katika lile banda letu. Ninashauri kwamba chumba kwajili ya kuetamia kiwe chumba cha kwanza au cha mwisho katika mfuatano wa vyumba vya banda lako. Andaa viota bora vya kuetamia, weka mayai 20 kwa kila kiota, ikiwa hayajatimia unaweza kununua kwa wafugaji wengine ili kuifikia idadi yako.

Waamishe kuku kutoka wanapotagia na kuwaweka katika chumba ulichokiandaa kwajili ya kuetamia. Ili ufanikiwe katika zoezi hili inafaa lifanyike wakati wa usiku na unafanya katika giza. Mweke kuku katika kila kiota na asubuhi wajikute kila mmoja katika kiota chake. Wahudumie kwa chakula na maji ya kutosha. Wakati wa usiku waongezee joto la ziada kwa kuweka jiko au ndoo ya chuma yenye chengachenga za mkaa au kama una umeme weka taa za joto.

Baada ya siku 21-25 kuku wako wataanza kuangua vifaranga. Huu ndio wakati unaotakiwa kuwa karibu sana na kuku wako kuliko wakati wote. Watenge vifaranga mara tu baada ya kuanguliwa; waweke katika chumba chao maalumu mbali na kuku. Kama chumba cha kuetamia kilikuwa cha kwanza basi vifaranga wawe chumba cha mwisho n.k

Ukishawatenga vifaranga mbali na matetea wako, wawekee tena mayai mengine 20 kila tetea, mayai ambayo utayanunua kwa wafigaji wenzako. Hakikisha kuku waliotaga hayo mayai ni wazuri, hawana magonjwa na wanauzito/ukubwa unaofaa. Mayai yote yakaguliwe vizuri ili kujua kwamba yameharibika, yana nyufa au mabovu. Kabla ya kuweka mayai mengine hakikisha chumba chako ni kisafi na viota vimesafishwa, havina wadudu na uchafu wowote. Kuku wako bila kujijua wataanza kuetamia upya mayai uliowawekea.

Ukiwawekea mayai rudia mzunguko kama nilivyokwambia awali. Baada ya siku 21 hadi 25 tena utapata vifaranga wako wengine tena. Fuata kila hatua kama nilivyokwambia hapo awali. Lakini kwa awamu hii nashauri waache matetea wako wapumzike wala usiwapatie mayai mengine tena.

JINSI YA KULEA VIFARANGA

Ikikaribia siku ya 20 tangu ulipowawekea matetea wako mayai katika chumba cha kuetamia, andaa chumba kwa ajili ya kulea vifaranga. Safisha kwa kuondoa uchafu na wadudu wote.

Washa taa ya joto au weka chombo cha kutoa joto katika chumba cha vifaranga nusu saa kabla hujaIMG_20141114_104757anza kuingiza vifaranga wako. Weka pia chakula na maji ya kutosha katika vyombo vyenye umbile na ukubwa utakaowawezesha vifaranga kuvitumia. Tandaza magazeti, maboksi, makaratasi n.k katika sakafu ya chumba hicho. Hakikisha vifaranga wako hawajikusanyi sehemu moja maana wakifanya hivyo wengi wao watakufa ili ufanikiwe katika jambo hili, banda lako liwe la mduara katika kona zake.

Weka joto la kutosha. Joto la kutosha ni lile linalowafanya vifaranga watawanyike chini ya chanzo cha joto wakati kama joto limezidi vifaranya kukimbia mbali na chanzo cha joto na ikiwa joto halitoshi vifaranga hujukusanya chini ya chanzo cha joto.

Baada ya siku 3 utawapatia chanjo ya Gumboro na siku 7 wapatie chanjo ya New Castle, utarudia tena kuwapa chanjo hii baada ya mwezi mmoja kisha utafanya hivi kila baada ya miezi mitatu mitatu.

MAPATO YA MRADI WAKO

Katika uzazi wa kwanza utapata vifaranga 150 kwa wastani wa vifaranga 15 kwa kila kuku. Tuseme haujazingatia kanuni za ufugaji za makala hii ukapata vifaranga 100 yani wastani wa vifaranga 10 kwa kila kuku. Kisha baadaye wakakua wakafa kuku 50 yani watano kwa kila kuku utakuwa na jumla ya kuku 50.

Baada ya wiki 3 utapata tena kuku tufanye kwa mahesabu kama hayo hapo juu kwa hasara utakuwa na kuku wengine 50, na kufanya jumla ya kuku 100. Ikiwa kuku wako baada ya uzao wa pili uliwapumzisha kwa miezi miwili basi mwezi wa 3 utapata tena kuku vifaranga 100 na wiki 3 baadaye utapata wengine 100. Kwa mahesabu kama hayo awali wakikuwa utakuwa na kuku wengine 100 ambao watakuwa.

Baada ya miezi 6 utakuwa na kuku wakubwa wa uzao wa kwanza 50, uzao wa pili kuku 50 na utakuwa na kuku wenye umri wa miezi mitatu 50 wa uzao wa 3 na kuku wengine 50 wa uzao wa 4.

Katika kuku 100 wa uzao wa kwanza na pili, tufanye kuku 50 wawe matetea ukijumlisha na kuku 10 ulioanza nao mradi utakuwa na matetea 60. Ikiwa kila tetea atatotoa vifaranga 10 na vikakua vitano tu, mwishoni utakuwa na kuku 300 na baada ya miezi mitatu kuku wengine 900 toka katika kutoka kwa uzao wa kwanza, wapili na watatu. Hivyo mwaka wa pili utafunga na kuku si chini ya 1,200/= wanaotaga mayai.

Ukiuza majogoo yote 1,200/= kwa bei ya 8,000/= ili upate pesa ya kujenga miundombinu bora maana sasa utakuwa na kuku wengi wanaoendelea kuzaliana kwa kasi utapata pesa kiasi cha TZS 7,200,000/=. Sasa ongeza kuku wako wa kutaga hadi wafikie kuku 4,000 maana sasa utakuwa na pesa za kutosha kuendesha mradi wako.

IMG_20140309_101614Sasa ukiwa na kuku 4000 wa kienyeji wa kutaga mayai, ikiwa kuku 3000 tu watataga ukauza yai moja kwa bei ya haraka haraka ya TZS 250 tu, utapata TZS 750,000/= kwa siku ambayo sawa na TZS 22,500,000/= kwa mwezi na TZS 270,000,000/= kwa mwaka sawa sawa na 128,572 USD. Kumbuka mwamba makadilio haya niya chini sana. Ukifata kanuni zote kwa makini na maombi huku ukimtanguliza Mungu utafikia hata TZS 500,000,000/= kwa mwaka.

Kumbuka unapofanikiwa kupata mapato ya kila aina, umtolee Mungu zaka(x10%) ya mapato yako, pia ukatoe sadaka ambayo ni kubwa kuliko zaka na uwasaidie masikini na wahitaji.

Tunza kumbukumbu zako zote za fedha katika daftari maalumu kuhusu mapato na matumizi ya mradi wako. Pia hali ya kuku wako kuhusu tarehe za chanjo ya mwisho, siku walipoanza kuetamia, magonjwa yanayowasumbua mara kwa mara n.k
© Copyright UJASILIAMALI FURSA | Designed By Code Nirvana
Back To Top